Our website uses necessary cookies to enable basic functions and optional cookies to help us to enhance your user experience. Learn more about our cookie policy by clicking "Learn More".
Accept All Only Necessary Cookies

Sobre este Soma Quran

Tafsiri ya Alcorão kwa Lugha ya Pamoja kiswahili na ufafanuzi esteira.

Tarjama hii imeandaliwa kwa lengo la kuwawezesha wazungumzaji wa Kiswahili kufahamu maana sahihi ya Qur-aan Tukufu, nayo ni ya kwanza ya aina yake kwa kuwa inaendana na manhaj ya Nabiy wetu Muhammad (صلى لله عليه وآله سلم) na Salafus-Swaalih; Maswahaba (رضي الله عنهم), Taabi’iyn na waliowafuata kwa ihsaan mpaka Siku ya mwisho.

Kuna mambo mengi yanayoimaizi Tarjama hii kulinganisha na Tarjama zingine za Kiswahili. Kati ya mambo hayo ni:

Imezithibitisha Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) zinazolaikiana na Utukufu Wake kama Alivyojithibitishia Yeye Mwenyewe na kuthibitishiwa pia na Rasuli Wake (صلى الله عليه آله وسلم) kama Sifa ya ‘Uluww (Kuweko juu), Istiwaa, Kusikia, Kuona, Mikono, Kuzungumza na Sifa nyinginezo zilizothibiti bila kuzifanyia ta'twiyl (kuzipinga, kukanusha uwezekano), wala tamthiyl (kumithilisha, kulinganisha), wala takyiyf (kuainisha; namna gani), wala tahriyf (kupotosha na kubadilisha maana), kama vile inavyojulikana katika ‘Aqiydah ya Ahlus Sunnah wal Jamaa’ah..

Imethibitisha masaail yote yahusianayo na mambo yaliyofichika (ghayb) kama Waumini kumwona Rabb wao Siku ya Qiyaamah na Peponi. Pia adhabu ya kaburi, Asw-Swiraatw (Njia ya kuvuka watu Siku ya Qiyaamah), Al-Miyzaan (Mizani) na mengineyo yaliyotajwa kwenye Qur-aan ‘Adhimu.

Tumechagua kwa uangalifu mkubwa misamiati inayowafikiana na makusudio ya Aayah.

Tumefafanua baadhi ya vipengele vinavyohitajia kufafanuliwa kama masaail ya ki-‘Aqiydah na kadhalika.

Tumeweka sababu za kuteremshwa baadhi ya Aayah au Suwrah na mafunzo yanayopatikana.

Tumetaja An-Naasikh (kinachofuta) na Al-Mansuwkh (kinachofutwa) pale tulipoweza.

Kazi yoyote ya mwana Aadam bila shaka haikosi kasoro, nasi kwa Tawfiyq ya Allaah tumejitahidi kiasi cha uwezo wetu kuepuka hilo. Tunamwomba yeyote atakayegundua kosa, au kasoro, au mponyoko wowote ndani ya Tarjama hii, asisite kutujulisha haraka awezavyo, nasi tutashukuru kwa hilo. Atujulishe kupitia barua yetu pepe: [email protected]

Tunamwomba Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Fadhila Zake, Ukarimu Wake, Upaji Wake, na Ihsani Yake, Atutakabalie kazi hii, hakika Yeye ni Mpaji Mno na Mkarimu Mno.

Traduzindo...

Informações Adicionais do Aplicativo

Última versão

Pedido Soma Quran Atualização 1.8

Enviado por

Farzana Hasin

Requer Android

Android 4.0.3+

Mostrar mais

Novidades da Última Versão 1.8

Last updated on Jul 21, 2019

Minor bug fixes and improvements. Install or update to the newest version to check it out!

Mostrar mais

Soma Quran Capturas de tela

Carregando Comentário...
Idiomas
Inscrever-se no APKPure
Seja o primeiro a ter acesso ao lançamento antecipado, notícias e guias dos melhores jogos e aplicativos para Android.
Não, obrigado
Inscrever-se
Inscreva-se com sucesso!
Agora você está inscrito no APKPure.
Inscrever-se no APKPure
Seja o primeiro a ter acesso ao lançamento antecipado, notícias e guias dos melhores jogos e aplicativos para Android.
Não, obrigado
Inscrever-se
Sucesso!
Agora você está inscrito em nossa newsletter.