Jifunze Kusoma Kiarabu


1.0 oleh Mahmoud Al-Asmi
Jan 3, 2018 Versi Lama

Mengenai Jifunze Kusoma Kiarabu

Belajar membaca dan menulis kepada Khati Bersatu.

Kwa Jina La Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

Kusoma na kuandika kwa khati za Kiarabu ni jambo jepesi. Wazee wetu wa Kiswahili waliokuwa visiwani Unguja, Pemba, Mombasa, Lamu na Mafia na waliokuwa mrima na mwambao wote wa Afrika Mashariki na katika miji ya asli ya Bara kama Tabora na Kigoma, karibu wote walikuwa wakijua kusoma Kuruani na wakijua kuandika na kusoma Kiswahili wakitumia harufi za Kiarabu kabla ya kufika mkoloni na kuleta Jifunze Kusoma Kiarabu

hizi harufi za Kizungu zinazotumiwa sana hivi sasa. Walipofika Wazungu wa mwanzo nchi ya Uganda waliwakuta watawala wenyeji wakiandikiana wao kwa wao kwa maandishi ya Kiarabu. Yamkini wakitumia Kiarabu au Kiswahili kwa maandishi ya Kiarabu. Lugha ya Kiarabu ni moja katika lugha kubwa za dunia. Ni lugha iliyoandikiwa vitabu vingi sana na ilimu za kila aina, lakini khasa ni lugha ya Waislamu wote katika dini yao, na lugha ya sehemu kubwa kabisa katika Bara la Afrika. Harufi za Kiarabu zinafuatana zaidi na matamshi fasihi ya lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo mwenye kujua kusoma na k'uandika kwa harufi ya Kiarabu, ataweza kusoma Kuruani kwa namna ilivyoteremka kwa Mtume S.A.W.,

na pia kitatengenea Kiswahili chake kiwe fasihi zaidi.

Yafaa kabla ya kuanza kusoma tujue kuwa Kiarabu kinaanza kulia kuendea kushoto, kinyume na maandishi ya Kizungu. Tena harufi zisizotamkwa bali zasaidia kutamka, vokali, haziitwi harufi, bali huitwa irabu kama A,I,U zinapokuja baada ya Konsonanti. Hizo konsonanti, kama B, T, R, H, M, N, D, Z, K n.k. ndizo zinazoitwa harufi.

Maklumat APLIKASI tambahan

Versi Terbaru

1.0

Dimuat naik oleh

مصطفى امين

Memerlukan Android

Android 4.0+

Tunjukkan Lagi

Jifunze Kusoma Kiarabu Alternatif

Dapatkan lebih banyak daripada Mahmoud Al-Asmi

Cari