關於Mwongozo wa Bembea ya Maisha
Mwongozo wa Bembea ya Maisha uliofanywa kueleweka barabara
Bembea ya Maisha ni hadithi kuhusu Yona na mkewe Sara pamoja na Bunju na mkewe Neema。 Wahusika hawa wanajikuta katika vuta n’kuvute inayochochewa na mitazamo ya kitamaduni,uhalisia wa mambo pamoja na matamanio ya wahusika binafsi。 Baina yao kuna mitikiso inayotishia familia,ndoa na mahusiano ya kijamii。 Kuna shutma,shaka,tuhuma na mivutano。 Lakini pia kuna hongera、imani、usrikiano、upendo、kutanabahi na mshikamano。 Katika huu mseto wa mambo ipo sauti imara ya Sara inayosika ikihimiza na kuzindua。 Sauti inayoiona kila hali mfano wa bembea。
Mwongozo wa Bembea ya Maisha utakupa tu mwelekeo lakini sharti kusoma vitabu vingine。
Ushauri muhimu kwa mtahiniwa。
1) Mtahiniwa sharti asome kitabu husika (Bembeaya Maisha) barabara na kukielewa。
2) Mwongozo ni kurunzi ya kumulikia njia, kwa hivyo, mtahiniwa sharti aelewe aendako。
3) Ni muhimu kusoma na kulielewa swali lililoulizwa。 Ni vyema kujiuliza swali lifuatalo:Mtahini anataka habari gani kutokana na swali hili?
4) Usitoke nje ya muktadha wa swali na kuandaa habari ambazo hazihusiani na swali uliloulizwa。
5) Ikiwezekana, toa mifano kutoka kwenye tamthilia inayohusiana na jambo unalolifafanua ili kuweka jambo hilo wazi。